Madaktari wapiga magoti kumuomba Rais aongeze muhula wa uongozi

Madaktari nchini Uganda wamempigia magoti Rais wao Yoweri Museveni wakimuomba kuongeza muhula mwingine wa kuwa Rais wa Taifa hilo wakisema ameboresha na kubadilisha sekta ya afya ikiwemo ustawi wa wafanyakazi wanaotoa huduma za matibabu.

Tukio hilo la Desemba 3, 2022, limetokea katika Viwanja vya Uhuru Kololo jijini Kampala, wakati wa kongamano la Vijana na Uwekezaji ambapo Rais Museveni alikuwa mgeni rasmi ambapo Rais wa Chama Cha madaktari Uganda Dkt. Odingo alimsifia Rais Museveni Kwa kuboresha huduma za afya nchini humo.

Amesema, “Umeboresha Hospitali za rufaa za mikoa, Hospitali kuu zinapandishwa hadhi hadi kufikia kiwango cha Hospitali za rufaa za mikoa, Watu wetu wanaweza kupokea huduma katika maeneo yao mahususi.”

Comments