WAZIRI WA HABARI,VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA SHULE ZA SEKONDARI JIJINI DAR ES SALAAM.

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Dk. Fenella Mukangara (wa kwanza kushoto)  na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom (wa pili kushoto), Salum Mwalim,Wakikabidhi baadhi ya vifaa vya michezo kwa mwanafunzi wa shule ya sekondari Mnazi Mmoja, Shaha Bakari(kulia)Vifaa hivyo vilivyotolewa na Vodacom Tanzania kwa ajili ya mashindano yatakayoanza hivi karibuni yatahusisha shule za sekondari kumi na mbili(12)za jijini Dar es Salaam.Akishuhudia makabidhiano hayo wapili kutoka kushoto ni Mwalimu michezo wa shule hiyo, Alex Dumien.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Dk. Fenella Mukangara (kushoto)Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania (wa pili kushoto), Salum Mwalim wakikabidhi vifaa vya michezo kwa mwanafunzi wa shule ya sekondari Mugabe, Juma Shabani (kulia)Vifaa hivyo vimetolewa na Vodacom Tanzania kwa ajili ya mashindano yatakayo anza hivi karibuni na kuhusisha shule za sekondari kumi na mbili(12) za jijini Dar es Salaam.Akishuhudia wapili kutoka kushoto ni Mwalimu wa shule hiyo, Farouk Kaburwa.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Dk. Fenella Mukangara(wapili toka kushoto)akishuhudia Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania(kulia) Salum Mwalim akikabidhi mfano wa hundi ya Milioni moja(1,000,000) kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Henry Lihaya (wa pili kushoto) fedha hizo zitatumika katika maandalizi wakati wa mashindano ya michezo shule za sekondari za Mkoa wa Dar es Salaam.Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Prof. Elisante Ole Gabriel.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Dk. Fenella Mukangara (wa pili kushoto)akikabidhi moja ya vifaa vya michezo kwa mwanafunzi wa shule ya sekondari Kibasila, Simon  Nungu (kulia)Vifaa hivyo vya michezo vilivyotolewa na Vodacom Tanzania kwa ajili ya mashindano ya michezo mbalimbali itakayoanza hivi karibuni na kuzihusisha shule za sekondari kumi na mbili(12)za jijini Dar es Salaam.Wanaoshuhudia makabidhiano hayo kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Prof. Elisante Ole Gabriel, Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania(wa tatu kushoto),Salum Mwalim.

Comments