Monalisa aelezea ‘bifu’ la Wema na Riyama Halijaanza kwenye Tuzo

Baada ya tuzo zile za  SZIFF kulikua na ka beef kati ya Wema Sepetu na Riyama ,ambapo kwenye tuzo hizo Wema alipata tuzo mbili .

Msanii mkongwe wa Bongo Movie Monalisa amesema kwamba Riyama hakua tu analalamika sababu ya tuzo alizoshinda Wema kulikua na mengine .

Lakini Wema na Riyama walionekana pamoja wakia poa tu kwenye  kumpokea Monalisa akitokea Nigeria ambapo alishinda tuzo ya The African Prestigious Awards (APA) 2017 kwenye kipengele cha Msanii Bora wa Kike barani Afrika.

“Kwanza niseme nilivyofika pale sikutegemea kuona watu lakini nilivyoshuka nikakutana na wasanii wenzangu, nilijisikia furaha sana,” amesema Monalisa.
“Nilifurahi kuawaona, sidhani kama Riyama kamlalamikia Wema nyie tu ndio mnachukulia vibaya, Riyama alikuwa na malalamiko yake na mimi ninayafahamu toka siku ya kwanza,” Monalisa ameiambia Times FM.
Ameongeza kuwa Riyama na Wema wote ni rafiki zake na anaongea nao vizuri na wote si watu wa vinyongo.

Comments