Benki ya CRDB yatekeleza kwa vitendo ahadi ya Rais Samia ya kufungua uchumi

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) akiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Proparco, Françoise Lombard, wakati alipotembelea Makao Makuu ya AFD jijini Paris, Ufaransa. Ujumbe wa Benki ya CRDB ulikutana na kampuni ya Proparco kujadili maeneo ya kimkakati ya ushirikiano na fursa za uwekezaji nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Idara ya Kilimo na Teknolojia ya Chakula wa taasisi ya Business France, Laure Elsaesser wakati wa ziara yake nchini Ufaransa. Ujumbe wa Benki ya CRDB upo nchini Ufaransa kukutana na wadau mbalimbali ili kuendeleza uhusiano na kujadili fursa za uwekezaji nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa SH Biaugeaud, Emmanuel Vallantin Dulac, wakati wa mkutano wa kujadili fursa za uwekezaji katika sekta ya kilimo Tanzania. Ujumbe wa Benki ya CRDB upo nchini Ufaransa kukutana na wadau mbalimbali ili kuendeleza mahusiano na kujadili fursa za uwekezaji nchini.





Comments