Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amesema, serikali ilishindwa kupeleka mapendekezo ya mabadiliko ya sheria ya habari bungeni katika Bunge la Novemba mwaka huu, kutokana na baadhi ya taratibu kutokamilika.
Akizungumza na uongozi wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), na Wadau wa Haki ya Kupata Habari (CoRI), jijini Dodoma Nape amesema Serikali ilitarajia kupeleka mapendekeo hayo lakini haikufanya hivyo kwa kuepuka mivutani kutoka kwa wadau wa habari.
Comments
Post a Comment