Jumla ya watu 14 wamefariki dunia, baada ya kutokea kwa shambulizi la ghafla katika msafara wa kijeshi wa waasi, wanaoungwa mkono naSerikali ya Iran katika eneo la mashariki mwa Syria lililo karibu na mpaka wa nchi ya Iraq.
Kwa mujibu wa Shirika la Syrian Observatory for Human Rights, linalofuatilia haki za binadamu nchini Syria, lenye makao yake nchini Uingereza limesema shambulizi hilo limefanywa katika malori yaliyokuwa yamebeba mafuta na silaha eneo la Albu Kamal.
Comments
Post a Comment