Serikali imeshauriwa kujiridhisha na umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia na iwapo imejipanga kukabili madhara yanayoweza kujitokeza ya watu kukosa ajira na kufa kwa viwanda vidogovidogo vya uzalishaji nchini.
Hayo yamebainishwa na Mshiriki wa mjadala wa Kitaifa wa Nishati safi ya kupikia Prof. Ishengoma hii leo Novemba 2, 2022 jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa ipo haja ya kujiuliza swali Nishati safi ya kupikia ni ipi licha ya kwamba ina mambo mengi mazuri lakini ambayo si salama.
Amesema, “Mimi leo nawachokoza na hoja zangu je unataka tuhamie kwenye gesi ni sawa lakini kuhama huku unaharibu ajira za watu wangapi, na baada ya hapo watu hawa watafanya nini na je nishati safi ya kupikia ni ipi haya ni mambo ya msingi ya kujiuliza.”
Comments
Post a Comment