Uwanja wa Ndege wa Bukoba ni salama: TCAA

Pamoja na kutokea kwa ajali ya ndege mali ya Precision Air Novemba 6, 2022 Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), imesema Uwanja wa Ndege wa Bukoba upo salama huku ikiwatoa hofu Watanzania wanaotumia usafiri wa Ndege kuelekea Kagera.

Amesema ajali hiyo iliyotokea Novemba 6 mwaka huu baada ya ndege hiyo kuanguka Ziwa Victoria karibu na uwanja huo na kusababisha vifo vya watu 19 na 24 kunusurika ilikuwa bahati mbaya huku akisema katika sekta ya anga tukio lolote linalotokea ni funzo ili kuhakikisha halijitokezi kwa mara nyingine.

Comments