TUSOME VITABU RADIO PROGRAME (HABARI NJEMA SANA KWA WATUNZI NA WAANDISHI WA VITABU TANZANIA)...!!!


TUSOME  VITABU  ni  kipindi  kipya  cha  redio  kitakacho   kujia  hivi  karibuni  kupitia   kituo  chako  cha  redio  ukipendacho  '" PASSION  FM " cha  jijini  Dar  es  salaam. Madhumuni  ya  kipindi  ni  kuwaelimisha  na  kuwahamasisha  watanzania  umuhimu  wa  kusoma  vitabu.  Na  Malengo  ya  kipindi  hiki  ni  kutengeneza  jamii  ya  watanzania  wenye  kupenda  na  kuthamini  kusoma  vitabu . Tutakuwa  tukifanya  mahojiano  na  waandishi pamoja  na  watunzi  mbalimbali  wa  vitabu  bila  kusahau  kuvifanyia  uchambuzi  wa  kina  vitabu  hivyo. Kama  wewe  ni  mwandishi  ama  mtunzi  wa  vitabu   na  ungependa  kushiriki  katika  kipindi  hiki  tafadhali  wasiliana  na  waandaaji  wa  kipindi  kwa  simu  namba :  0767010756.   Tunakaribisha  watunzi  wa  vitabu  vya  aina  zote, yaani  vitabu  vya  ziada  na  kiada, vitabu  vya  kitaaluma   na  vitabu   viusivyokuwa  vya  kitaaluma.Ewe  mwandishi , ewe  mtunzi  wa  vitabu, tumia   nafasi  hii  ya  pekee  kutangaza  kitabu  chako. Usibakie  kusema  tu  "  Watanzania  ni  wavivu  wa  kusoma  vitabu  wakati  hujakitangaza  kitabu  chako "KWA  MAELEZO ZAIDI  WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA :  0767010756

Comments