PISHI LA LEO: CHAPATI ZA MAJI/MAYAI by LADY JAY DEE...!!!

Jinsi ya kutengeneza Pancakes

Mahitaji:
Unga wa ngano 500g
Mayai 2
Sukari tablespoon 3
Chumvi teaspoon 1/2
Kitunguu  1/2  (kata vipande vidogo vidogo sana)
Hiliki 1/4 teaspoon (iliosagwa ikawa unga)
Siagi (kama Blueband au inayofanania na hiyo) 

Hatua ya kwanza unapasua mayai, kisha unayakoroga katika chombo chenye nafasi ya kutosha.

Unaweka kitunguu mara tu baada ya mayai
 
Unaweka chumvi na sukari unaendelea kukoroga
Huku ukiweka unga wa ngano kidogo, kidogo
Na unakuwa unaongeza na maji taratibu
Huku ukiangalia uzito wa uji
Usiwe mzito sana, wala mwepesi sana
Piga piga mpaka uhakikishe mabonge bonge yote yamekwisha
Weka hiliki koroga tena

Baada ya hapo utakuwa umepata mchanganyiko wa kutengenezea Pancakes.
Weka kikaango katika moto wa wastani
Majiko yanatofautiana settings
Kwahiyo basi, kutokana na jiko lako moto uwe wa kati

Jinsi ya kuzipika:
Unaweka siagi kwenye kiaango
Unamimina unga unaacha mpk ukauke
Kabla ya kugeuza upande wa pili unapaka tena siagi
Pancake haichomwi zaidi ya dakika 3

Kwa kipimo hicho unaweza kupata Pancake 20-25
Ukitaka pungufu unakata vipimo nilivyoelezea nusu yake
Ambapo unaweza kupata Pancakes 10-12

Nawatakia Jumapili Njema.

Comments