MAMA MZAZI WA MTOTO ALIYEKATWA MKONO AWASHUKURU WAKAZI WA MBEYA NA MAJIRANI WALIOTOA TAARIFA YA KUTESWA KWA MTOTO WAKE...!!!
Mama mzazi wa mtoto Aneth Bi Asera Mkandara akiwa hospitali akimuuguza mwanae
Mtoto Aneth akiwa hospitalini hapo na kwa sasa hali yake inaendelea vizuri
Mama Mzazi wa Aneth akiongea na mwandishi wa gazti la majira Rashid Mkwinda hospitalini hapo
Umati wa wakazi wa Mbeya wanaoenda hospitalini hapo kumuona mtoto Aneth.
---
---
MAMA wa mtoto Aneth Johanes aliyefanyiwa unyama na hatimaye kukatwa mkono Asera Mkandara ametoa shukurani kwa wananchi wa Mbeya na majirani waliosaidia kutoa taarifa na hatimaye kuokoa maisha ya mwanaye aliyekuwa akiishi kwa mateso.
Bi. Mkandara alizungumza hayo alipotembelewa na wanahabari waliofika wodi namba 8 kumjulia hali mtoto Aneth na kusema kuwa alipewa taarifa za kutokea kwa matatizo ya mwanaye lakini hakufafanuliwa ni tatizo gani alilopata.
Anasema kuwa amewasili Jijini Mbeya akitokea kwao Muleba Bukoba na kumkuta mwanaye Aneth ambaye ni mtoto wake wa pili baada ya mwanaye wa kwanza mwenye umri wa miaka 7 anayelelewa na bibi yake mjini Bukoba.
Anasema kuwa hata hivyo yeye hana shughuli maalumu zinazomuendeshea maisha yake isipokuwa biashara ndogo ndogo hivyo kuchukuliwa kwa mtoto wake na kaka yake aliyemtambulisha kwa jina moja la Mkandara ilikuwa ni sehemu ya msaada kwake.
Mama huyo anafafanua kuwa anashukuru kukuta mwanaye ni mzima na anawashukuru madaktari waliompa msaada kwani inawezekana huduma za matibabu zingechelewa angeweza kupata madhara makubwa.
Anasema kuwa kwa sasa anasaidiwa na ndugu na majirani na baadhi ya watu wanaomiminika hospitalini hapo kutoa msaada.
YEYOTE MWENYE MAPENZI MEMA ANAWEZA KUTOA MSAADA KUPITIA NAMBA YA SIMU YA MKONONI YA MAMA HUYO 0756-293784
Habari na picha kwa hisani ya Mbeya Yetu Blog
Comments
Post a Comment