OFA ZAIDI KWA MSHINDI
Mbali na mshindi kuondoka na gari, Mrisho aliongeza kuwa washindi watatu wa nafasi za juu watajipatia dili la kurekodi singo mojamoja kutoka kwa prodyuza kiwango aliyezalisha ngoma kali Bongo ikiwemo ya Kundi la Kigoma All Stars iitwayo Leka Dutigite, Tudd Thomas.
TUZO KUTOLEWA
Mrisho alitiririka na mistari kuwa, mbali na shoo kali kutoka kwa wakali hao wa Hip Hop, kutakuwa na kipengele cha kutoa tuzo za muziki wa Hip Hop katika vipengele tofauti hivyo mashabiki pia waendelee kuwapigia kura wasanii wanaowapenda.
Vipengele vitakavyotolewa tuzo ni Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Legendary) ambapo yamepita majina matatu; Fid Q, Joh Makini na Profesa Jay. Pia kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Chipukizi) ambacho kina majina kama Young Killer, P The Mc na Tabla huku akianisha kipengele cha mwisho ambacho ni Wimbo Bora wa Hip Hop (2012/13) chenye nyimbo kali za Dear God (Kala Jeremiah), Sihitaji Marafiki (Fid Q) na Najuta Kubalehe (Stamina).
“Ili kuwapigia kura, mashabiki wanatakiwa kuandika neno BHL wakiambatanisha na jina la msanii husika kwenda namba 15564 katika kipengele cha Msanii Bora wa Hip Hop (Legendary).
“Kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Chipukizi), mashabiki waandike neno BUA na kufuatiwa na jina la msanii wanayempenda kwenda namba 15564,” alisema Abby Cool na kuongeza:
“Kipengele cha Wimbo Bora wa Mwaka, mashabiki waandike neno BHS likifuatiwa na jina la msanii wanayempenda kisha watume ujumbe huo kwenda namba 15564.”
KUWAENZI WASANII/SOKA KWENYE SKRINI KUBWA
Abby Cool aliweka bayana kuwa katika shoo hiyo kutakuwepo na documentary maalumu ya kuwakumbuka wasanii wa Hip Hop waliotangulia mbele za haki kupitia skrini kubwa bila kusahau mashabiki wa soka watapata fursa ya kushuhudia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (Uefa) kati ya Bayern Munich na Borrusia Dortmund. Twendeni Dar Live J’mosi!
Comments
Post a Comment