WATEJA GNLD SASA KULIPIA BIDHA KWA NJIA YA M-PESA.

Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Rukia Mtingwa akimsikiliza jambo na Mkurugenzi wa Timu ya Dunia wa wa kampuni inayohusika na uuzaji wa dawa asilia zenye ubora wa kimataifa ya GNLD Tanzania,Bi.Grace Rubambey,mara baada ya hafla ya kuwawezesha wateja wa kampuni hiyo kuanza kulipia bidhaa mbalimbali  zenye ubora wa kimataifa kupitia huduma ya M-Pesa.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria halfa hiyo ya kuwawezesha wateja wa kampuni ya GNLD kuanza kulipia bidhaa mbalimbali  zenye ubora wa kimataifa kupitia huduma ya M-Pesa. 
Mmoja wa wateja wa  kampuni inayouza bidhaa za asilia pamoja na dawa zenye ubora wa kimataifa (GNLD)akiuliza swali juu ya ulipaji pesa kupitia huduma ya M-PESA,wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Meneja Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Rukia Mtingwa(kushoto) pamoja na Mwakilishi wa GNLD Tanzania, Daniel Mutiso,wakipongezana mara baada ya kukamilisha makubaliano ya kibiashara na kampuni inayohusika na uuzaji wa dawa asilia zenye ubora wa kimataifa ya GNLD Tanzania,ambayo itawawezesha wateja wa kampuni hiyo kulipia Ankara zao kupitia huduma ya  M-PESA.
Vodacom Tanzania Corporate Communications Manager, Rukia Mtingwa (left) shows the steps to be used when purchasing GNLD products through M-Pesa. Vodacom Tanzania has entered into a partnership with GNLD that will see GNLD customers pay for products through M-Pesa.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Wateja GNLD sasa kulipia bidhaa kwa njia ya M-Pesa Dar es Salaam, Mei 6, 2013 ... WATEJA wa huduma ya M-Pesa nchini sasa watanufaika na huduma hiyo ya teknolojia ya simu kwa kuwawezesha watanzania kwa mara ya kwanza kulipia bidhaa za kampuni ya GNLD Tanzania inayouza dawa asilia zenye ubora wa kimataifa kupitia huduma hiyo ya M-Pesa.

Huduma ya M-Pesa, imeendelea kurahisisha maisha ya watanzania kwa kupanua huduma zake katika sekta mbalimbali za kibenki wakati huu ikishuhudia kuingia katika ushirikiano kati ya Kampuni ya Vodacom Tanzania na Kampuni inayohusika na uuzaji wa dawa asilia zenye ubora wa kimataifa ya GNLD Tanzania. Mpango huu umelenga kunufaisha wateja kwa kuweza kulipia bidhaa za GNLD kwa njia ya huduma hiyo ya M-Pesa.

Kwa mujibu wa Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Rukia Mtingwa, wateja ambao wako tayari kulipa kwa ajili ya bidhaa za GNLD hawana sababu tena ya kubeba fedha kwa sababu za usalama.

"M-Pesa ni huduma ambayo ni salama na ya haraka. Kutokana na ushirikiano huu, wateja hawatakuwa na sababu ya kupoteza muda wao kwenda kwa wakala wa GNLD kulipa kwa ajili ya bidhaa fulani. Wanachotakiwa kufanya ni kutumia huduma ya Vodacom M-Pesa na kufanya malipo," anasema Mtingwa.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa GNLD Tanzania, Daniel Mutiso, anasema kwamba GNLD itaendelea kuhakikisha kwamba inaendelea kutoa huduma yenye kiwango cha juu cha ubora ili kukuza afya bora kwa kila mtu.

"Ushirikiano huu ni wa kwanza na wa aina yake katika soko hili. Hivyo tunajisikia furaha kufanya uzinduzi huu leo kwasababu utaweza kusaidia kila mtu katika nchi hii," anasema Mutiso.
Kulipia bidhaa za GNLD kupitia huduma ya M-Pesa, wateja watakiwa kupiga *150*00# na kuchagua  Malipo na kisha kuingiza namba ya Biashara ambayo ni 000221na kufuatiwa na namba ya akaunti ikifuatiwa na Kiasi kisha Namba ya Siri (PIN) na mwisho kufanya uthibitisho.

Comments