Dk. Charles Kimei akisaini kitabu cha wageni Ubalozini Tanzania House,Washington DC.
Mazungumzo yakiendelea yaliyomshirikisha Dk.Kimei, Maofisa wake Waandamizi kutoka CRDB, Bw.Shumake na Mhe.Balozi Mulamula.
Dk. Kimei akimkabidhi Bw. Shumake zawadi ya kumbukumbu kutoka benki ya CRDB.
Dk.Kimei akimkabidhi Mhe.Balozi Liberata Mulamula zawadi kutoka benki hiyo.
Mhe.Balozi Mulamula akiwa katika picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk.Charles Kimei. Wengine kushoto ni Bw. Kenneth Kasigila,Msaidizi wa Dk. Kimei na Bw. Alex Ngusaru, Mkurugenzi wa Hazina CRDB na Bw.Suleiman Saleh,Afisa wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC.
Kwa upande mwingine Dk. Charles Kimei alipata fursa ya kufanya mazungumzo na Bw. Robert Shumake, Balozi wa Heshima wa Tanzania katika jimbo la Michigan ambayo yalihudhuriwa pia na Mhe.Balozi Liberata Mulamula. Mazungumzo baina ya Dk. Kimei na Bw. Shumake yalijikita zaidi katika kuainisha maeneo ya mashirikiano kati ya Benki ya CRDB na Kampuni ya Shumake Global Partners ya Bw. Shumake yenye makao yake Detroit,Michigan. Katika mazungumzo hayo baina Bw.Shumake na Dk.Kimei yalihudhuriwa pia na Bibi Tully M., Mkurugenzi wa Masoko wa CRDB, Bw.Alex Ngusaru Mkurugenzi wa Hazina (CRDB) na Bw.Kenneth Kasigila, Msaidizi wa Dk.Kimei.
Pichani Dk.Kimei katika taswira mbali mbali alipokuwa Ubalozini wa Tanzania Washington DC.
Comments
Post a Comment